Friday, April 13, 2012

KWENU NI KWENU

Hakuna aliyekuja duniani kwa bahati mbaya."Mimi nimezaliwa hapa kwa bahati mbaya" Utasikia mtu akitamba na kujisifia.Mungu hakukosea wewe kuzaliwa mahali ulipo.Alijua unahitajika kuwepo mahali ulipo.Wa namna yako hayupo dunia nzima.Angelikuwepo usingezaliwa.Kuna vitu vizuri ameweka ndani yako kwa ajili ya utukufu wake na kwa faida ya wengine.Usijidharau.Ona fahari ya Taifa lako.Tulia na kutafakari juu ya vitu vizuri ambavyo Mungu ameweka ndani yako.Mwombe Mungu akupe fursa ya kuchipuka na kutumika hata kwa kile ambacho wewe unaona ni kidogo.Tumia elimu,kipaji,utajiri na chochote ulicho nacho kama mchango na wajibu kwa dunia inayokuzunguuka.Furahi.Jinsi ulivyo ni pambo mbele za Mungu.Usijidharau.(Zaburi 139:14-18)

No comments:

Post a Comment